Mk. 13:31-34 Swahili Union Version (SUV)

31. Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

32. Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.

33. Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.

34. Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe.

Mk. 13