28. Kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake liishapo kuwa laini, na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno ni karibu;
29. nanyi kadhalika, myaonapo mambo hayo yanaanza, tambueni ya kuwa yu karibu milangoni.
30. Amin, nawaambieni, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatimie.
31. Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
32. Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
33. Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.