11. Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;
12. na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.
13. Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.
14. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.
15. Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.