Mk. 10:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;

12. na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.

13. Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.

14. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.

15. Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

Mk. 10