19. Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi,Na faida yangu hupita fedha iliyo teule.
20. Natembea katika njia ya haki,Katikati ya mapito ya hukumu.
21. Niwarithishe mali wale wanipendao,Tena nipate kuzijaza hazina zao.
22. BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake,Kabla ya matendo yake ya kale.
23. Nalitukuka tokea milele, tangu awali,Kabla haijawako dunia.
24. Wakati visipokuwako vilindi nalizaliwa,Wakati zisipokuwako chemchemi zilizojaa maji.
25. Kabla milima haijawekwa imara,Kabla ya vilima nalizaliwa.
26. Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makondeWala chanzo cha mavumbi ya dunia;