Mit. 7:7-14 Swahili Union Version (SUV)

7. Nikaona katikati ya wajinga,Nikamtambua miongoni mwa vijana,Kijana mmoja asiyekuwa na akili,

8. Akipita njiani karibu na pembe yake,Akiishika njia iendayo nyumbani kwake,

9. Wakati wa magharibi, wakati wa jioni,Usiku wa manane, gizani.

10. Na tazama, mwanamke akamkuta,Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;

11. Ana kelele, na ukaidi;Miguu yake haikai nyumbani mwake.

12. Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani,Naye huotea kwenye pembe za kila njia.

13. Basi akamshika, akambusu,Akamwambia kwa uso usio na haya,

14. Kwangu ziko sadaka za amani;Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;

Mit. 7