Mit. 7:18-25 Swahili Union Version (SUV)

18. Haya, na tushibe upendo hata asubuhi,Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.

19. Maana mume wangu hayumo nyumbani,Amekwenda safari ya mbali;

20. Amechukua mfuko wa fedha mkononi;Atarudi wakati wa mwezi mpevu.

21. Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi,Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.

22. Huyo akafuatana naye mara hiyo,Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni;Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;

23. Hata mshale umchome maini;Kama ndege aendaye haraka mtegoni;Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.

24. Basi, wanangu, nisikilizeni sasa,Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.

25. Moyo wako usizielekee njia zake,Wala usipotee katika mapito yake.

Mit. 7