17. Nimetia kitanda changu manukato,Manemane na udi na mdalasini.
18. Haya, na tushibe upendo hata asubuhi,Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
19. Maana mume wangu hayumo nyumbani,Amekwenda safari ya mbali;
20. Amechukua mfuko wa fedha mkononi;Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
21. Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi,Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.