Mit. 7:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Nimetia kitanda changu manukato,Manemane na udi na mdalasini.

18. Haya, na tushibe upendo hata asubuhi,Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.

19. Maana mume wangu hayumo nyumbani,Amekwenda safari ya mbali;

20. Amechukua mfuko wa fedha mkononi;Atarudi wakati wa mwezi mpevu.

21. Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi,Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.

Mit. 7