Mit. 6:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Ewe mvivu, mwendee chungu,Zitafakari njia zake ukapate hekima.

7. Kwa maana yeye hana akida,Wala msimamizi, wala mkuu,

8. Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua;Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

9. Ewe mvivu, utalala hata lini?Utaondoka lini katika usingizi wako?

10. Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,Bado kukunja mikono upate usingizi!

Mit. 6