16. Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA;Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo,Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18. Moyo uwazao mawazo mabaya;Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19. Shahidi wa uongo asemaye uongo;Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.
20. Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,Wala usiiache sheria ya mama yako.
21. Yafunge hayo katika moyo wako daima;Jivike hayo shingoni mwako.
22. Uendapo yatakuongoza, ulalapo yatakulinda,Na uamkapo yatazungumza nawe.