4. Naye akanifundisha, akaniambia,Moyo wako uyahifadhi maneno yangu;Shika amri zangu ukaishi.
5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau;Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu.
6. Usimwache, naye atakuhifadhi;Umpende, naye atakulinda.
7. Bora hekima, basi jipatie hekima;Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
8. Umtukuze, naye atakukuza;Atakupatia heshima, ukimkumbatia.