19. Njia ya waovu ni kama giza;Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho.
20. Mwanangu, sikiliza maneno yangu;Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu.
21. Zisiondoke machoni pako;Uzihifadhi ndani ya moyo wako.
22. Maana ni uhai kwa wale wazipatao,Na afya ya mwili wao wote.