9. Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki;Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.
10. Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?Maana kima chake chapita kima cha marijani.
11. Moyo wa mumewe humwamini,Wala hatakosa kupata mapato.
12. Humtendea mema wala si mabaya,Siku zote za maisha yake.