Mit. 31:16-23 Swahili Union Version (SUV)

16. Huangalia shamba, akalinunua;Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17. Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;Hutia mikono yake nguvu.

18. Huona kama bidhaa yake ina faida;Taa yake haizimiki usiku.

19. Hutia mikono yake katika kusokota;Na mikono yake huishika pia.

20. Huwakunjulia maskini mikono yake;Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

21. Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake;Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu.

22. Hujifanyia mazulia ya urembo;Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

23. Mume wake hujulikana malangoni;Aketipo pamoja na wazee wa nchi.

Mit. 31