10. Mke mwema, ni nani awezaye kumwona?Maana kima chake chapita kima cha marijani.
11. Moyo wa mumewe humwamini,Wala hatakosa kupata mapato.
12. Humtendea mema wala si mabaya,Siku zote za maisha yake.
13. Hutafuta sufu na kitani;Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
14. Afanana na merikebu za biashara;Huleta chakula chake kutoka mbali.