Mit. 30:24-29 Swahili Union Version (SUV)

24. Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo;Lakini vina akili nyingi sana.

25. Chungu ni watu wasio na nguvu;Lakini hujiwekea chakula wakati wa hari.

26. Wibari ni watu dhaifu;Lakini hujifanyia nyumba katika miamba.

27. Nzige hawana mfalme;Lakini huenda wote pamoja vikosi vikosi.

28. Mjusi hushika kwa mikono yake;Lakini yumo majumbani mwa wafalme.

29. Kuna watatu wenye mwendo wa kupendeza,Naam, wanne walio na mwendo mzuri.

Mit. 30