9. Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria,Hata sala yake ni chukizo.
10. Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya,Ataanguka katika rima lake mwenyewe;Bali wakamilifu watarithi mema.
11. Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe;Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.
12. Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi;Bali waovu waondokapo, watu hujificha.
13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa;Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
14. Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote;Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.
15. Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa;Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.
16. Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana;Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.
17. Aliyelemewa na damu ya mtuAtalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.
18. Aendaye kwa unyofu ataokolewa;Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.
19. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.
20. Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;Lakini afanyaye haraka kuwa tajiri hakosi ataadhibiwa.
21. Kupendelea watu si kwema;Wala mtu kuasi kwa ajili ya kipande cha mkate.
22. Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri;Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.
23. Amkemeaye mwenzake hatimaye atapata kibali;Zaidi ya mtu ajipendekezaye kwa ulimi wake.
24. Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa;Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.