Mit. 28:11-19 Swahili Union Version (SUV)

11. Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe;Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.

12. Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi;Bali waovu waondokapo, watu hujificha.

13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa;Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

14. Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote;Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.

15. Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa;Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.

16. Mkuu aliyepungukiwa na akili huwaonea watu sana;Bali achukiaye kutamani ataongeza siku zake.

17. Aliyelemewa na damu ya mtuAtalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.

18. Aendaye kwa unyofu ataokolewa;Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.

19. Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.

Mit. 28