10. Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya,Ataanguka katika rima lake mwenyewe;Bali wakamilifu watarithi mema.
11. Mtu tajiri ana hekima machoni pake mwenyewe;Bali maskini mwenye ufahamu humchunguza sana.
12. Wenye haki washindapo, uko utukufu mwingi;Bali waovu waondokapo, watu hujificha.
13. Afichaye dhambi zake hatafanikiwa;Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.
14. Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote;Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara.
15. Kama simba angurumaye, na dubu mwenye njaa;Ndivyo alivyo mtu mbaya awatawalaye maskini.