13. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoza rehani aliye mdhamini wa malaya.
14. Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema;Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.
15. Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi,Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;
16. Atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo;Na mkono wake wa kuume hukuta mafuta.
17. Chuma hunoa chuma;Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.
18. Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.
19. Kama uso ufananavyo na uso katika maji;Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.
20. Kuzimu na Uharibifu havishibi;Wala macho ya wanadamu hayashibi.