Mit. 27:13-20 Swahili Union Version (SUV)

13. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoza rehani aliye mdhamini wa malaya.

14. Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema;Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.

15. Kutona-tona daima siku ya mvua nyingi,Na mwanamke mgomvi ni sawasawa;

16. Atakaye kumzuia huyo huuzuia upepo;Na mkono wake wa kuume hukuta mafuta.

17. Chuma hunoa chuma;Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.

18. Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;Naye amhudumiaye bwana wake ataheshimiwa.

19. Kama uso ufananavyo na uso katika maji;Kadhalika moyo wa mtu na mwenzake.

20. Kuzimu na Uharibifu havishibi;Wala macho ya wanadamu hayashibi.

Mit. 27