1. Usijisifu kwa ajili ya kesho;Kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja.
2. Mwingine na akusifu wala si kinywa chako mwenyewe;Mtu mgeni wala si midomo yako wewe.
3. Jiwe ni zito, na mchanga hulemea;Lakini ghadhabu ya mpumbavu ni nzito kuliko hivi vyote viwili.
4. Ghadhabu ni kali, na hasira ni gharika;Lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu.
5. Lawama ya wazi ni heri,Kuliko upendo uliositirika.