13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.
14. Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake;Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake.
15. Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini;Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake.
16. Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake,Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.
17. Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake;Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.