Mit. 26:13-17 Swahili Union Version (SUV)

13. Mtu mvivu husema, Simba yuko njiani,Simba yuko katika njia kuu.

14. Kama vile mlango ugeukavyo katika bawaba zake;Kadhalika mtu mvivu katika kitanda chake.

15. Mtu mvivu hutia mkono wake sahanini;Kwamchosha kuupeleka tena kinywani pake.

16. Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake,Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.

17. Mtu apitaye na kujisumbua kwa ugomvi usio wake;Ni kama mtu ashikaye mbwa kwa masikio yake.

Mit. 26