Mit. 25:7-13 Swahili Union Version (SUV)

7. Kwa maana ni heri kuambiwa, Njoo huku mbele;Kuliko kuwekwa nyuma machoni pa mkuu.Yale uliyoyaona kwa macho,

8. Usitoke nje kwa haraka ili kuyashindania;Usije ukakosa kujua la kutenda hatimaye,Mwenzako atakapokuwa amekuaibisha.

9. Ujitetee na mwenzako peke yake;Bali usiifunue siri ya mtu mwingine;

10. Yeye asikiaye asije akakutukana;Na aibu yako isiondoke.

11. Neno linenwalo wakati wa kufaa,Ni kama machungwa katika vyano vya fedha.

12. Kipuli cha dhahabu, na pambo la dhahabu safi;Ndivyo alivyo mwonyaji mwenye hekima kwa sikio lisikialo.

13. Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;Ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao;Kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.

Mit. 25