1. Hizi nazo ni mithali za Sulemani, ambazo watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda, walizinakili.
2. Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo;Bali ni utukufu wa mfalme kuchunguza jambo.
3. Mbingu huenda juu sana, na nchi huenda chini;Lakini mioyo ya wafalme haichunguziki.
4. Ondoa takataka katika fedha,Na chombo kitatokea kwa mtakasaji;