7. Kwa mpumbavu hekima haipatikani;Hafumbui kinywa chake langoni.
8. Mtu afikiriye kutenda maovu,Watu watamwita mtundu;
9. Fikira za mpumbavu ni dhambi,Na mwenye mzaha huwachukiza watu.
10. Ukizimia siku ya taabu,Nguvu zako ni chache.
11. Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe;Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.
12. Ukisema, Sisi hatukujua hayo;Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye?Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye?Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?