Mit. 24:7-12 Swahili Union Version (SUV)

7. Kwa mpumbavu hekima haipatikani;Hafumbui kinywa chake langoni.

8. Mtu afikiriye kutenda maovu,Watu watamwita mtundu;

9. Fikira za mpumbavu ni dhambi,Na mwenye mzaha huwachukiza watu.

10. Ukizimia siku ya taabu,Nguvu zako ni chache.

11. Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe;Nao walio tayari kuchinjwa uwaopoe.

12. Ukisema, Sisi hatukujua hayo;Je! Yeye aipimaye mioyo siye afahamuye?Naye ailindaye nafsi yako siye ajuaye?Je! Hatamlipa kila mtu sawasawa na kazi yake?

Mit. 24