Mit. 24:20-24 Swahili Union Version (SUV)

20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.

21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

22. Maana msiba wao utatokea kwa ghafula;Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.

23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.

24. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki;Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.

Mit. 24