20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.
21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;
22. Maana msiba wao utatokea kwa ghafula;Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.
23. Haya nayo pia ni maneno ya wenye akili.Kupendelea watu katika hukumu si kwema.
24. Amwambiaye mtu mwovu, Wewe una haki;Kabila za watu watamlaani, taifa watamchukia.