Mit. 24:17-21 Swahili Union Version (SUV)

17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;

18. BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha;Akageuzia mbali naye hasira yake.

19. Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya;Wala usiwahusudu wabaya;

20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.

21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;

Mit. 24