17. Usifurahi, adui yako aangukapo;Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18. BWANA asije akaliona hilo, likamkasirisha;Akageuzia mbali naye hasira yake.
19. Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya;Wala usiwahusudu wabaya;
20. Kwa maana mtu mbaya hapati thawabu;Taa ya mtu mbaya itazimika.
21. Mwanangu, mche BWANA, na mfalme;Wala usishirikiane na wenye kigeugeu;