Mit. 24:13-16 Swahili Union Version (SUV)

13. Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema,Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.

14. Basi utaijua hekima kuwa tamu kwa nafsi yako;Ikiwa umekwisha kuiona;Ndipo itakapofuata thawabu;Wala tumaini lako halitabatilika.

15. Ewe mtu mbaya, usiyavizie makao yake mwenye haki;Wala usipaharibu mahali pake pa kupumzika;

16. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena;Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

Mit. 24