5. Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu?Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa,Kama tai arukaye mbinguni.
6. Usile mkate wa mtu mwenye husuda;Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;
7. Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo.Akuambia, Haya, kula, kunywa;Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
8. Tonge lile ulilokula utalitapika,Na maneno yako matamu yatakupotea.