30. Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo;Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.
31. Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu;Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu;
32. Mwisho wake huuma kama nyoka;Huchoma kama fira.
33. Macho yako yataona mambo mageni;Na moyo wako utatoa yaliyopotoka.
34. Naam, utakuwa kama alalaye katikati ya bahari;Au kama yeye asinziaye juu ya mlingoti.