17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;
18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.
19. Sikia, mwanangu, uwe na hekima,Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.
20. Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo;Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
21. Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini,Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
22. Msikilize baba yako aliyekuzaa,Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.