15. Mwanangu, kama moyo wako una hekima,Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;
16. Naam, viuno vyangu vitafurahi,Midomo yako inenapo maneno mema.
17. Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi;Bali mche BWANA mchana kutwa;
18. Maana bila shaka iko thawabu;Na tumaini lako halitabatilika.