Mit. 22:19-26 Swahili Union Version (SUV)

19. Ili matumaini yako uyaweke kwa BWANA, leo nimekujulisha wewe haya, naam, wewe.

20. Je! Sikukuandikia mambo makuu juu ya mashauri na juu ya maarifa;

21. ili kukujulisha hakika ya maneno ya kweli, uwarudishie wakutumao maneno ya kweli?

22. Usimnyang’anye maskini, kwa kuwa ni maskini;Wala usimdhulumu mtu mnyonge langoni;

23. Kwa sababu BWANA atawatetea;Naye atawateka uhai wao waliowateka.

24. Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi;Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;

25. Usije ukajifunza njia zake;Na kujipatia nafsi yako mtego.

26. Usiwe mmoja wao wawekao rehani;Au walio wadhamini kwa deni za watu;

Mit. 22