Mit. 21:8-14 Swahili Union Version (SUV)

8. Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana;Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.

9. Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini,Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.

10. Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu;Jirani yake hapati fadhili machoni pake.

11. Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima;Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.

12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.

13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.

14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.

Mit. 21