3. Kutenda haki na hukumuHumpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.
4. Macho yenye kiburi, na moyo wa kutakabari,Hata ukulima wa waovu, ni dhambi.
5. Mawazo ya wenye bidii huuelekea utajiri tu;Bali kila mwenye pupa huuelekea uhitaji.
6. Kupata akiba ya mali kwa ulimi wa uongoNi moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
7. Jeuri ya wabaya itawaondolea mbali;Kwa sababu wamekataa kutenda hukumu.
8. Njia yake aliyelemewa na dhambi imepotoka sana;Bali mtu aliye safi, kazi yake ni sawasawa.
9. Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini,Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.
10. Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu;Jirani yake hapati fadhili machoni pake.
11. Mwenye mzaha aadhibiwapo, mjinga hupata hekima;Na mwenye hekima afundishwapo, hupokea maarifa.
12. Mwenye haki huitafakari nyumba ya mtu mbaya;Jinsi wabaya waangushwavyo wakaangamia.
13. Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini,Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.
14. Kipawa cha siri hutuliza hasira;Na rushwa bindoni humliza ghadhabu kali.