8. Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu,Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.
9. Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu;Nimetakasika dhambi yangu?
10. Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali,Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.
11. Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.
12. Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.
13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.