Mit. 20:5-22 Swahili Union Version (SUV)

5. Mashauri ya moyoni ni kama kilindi;Lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.

6. Wanadamu hutangaza kila mtu hisani yake mwenyewe;Bali mtu aliye mwaminifu, ni nani awezaye kumpata?

7. Mwenye haki aendaye katika unyofu wake,Watoto wake wabarikiwa baada yake.

8. Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu,Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.

9. Nani awezaye kusema, Nimesafisha moyo wangu;Nimetakasika dhambi yangu?

10. Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali,Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.

11. Hata mtoto hujijulisha kwa matendo yake;Kwamba kazi yake ni safi, kwamba ni adili.

12. Sikio lisikialo, na jicho lionalo,BWANA ndiye aliyeyafanya yote mawili.

13. Usipende usingizi usije ukawa maskini;Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.

15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.

16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.

17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.

18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.

19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.

20. Amlaaniye babaye au mamaye,Taa yake itazimika katika giza kuu.

21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.

22. Usiseme, Mimi nitalipa mabaya;Mngojee BWANA, naye atakuokoa.

Mit. 20