Mit. 20:20-27 Swahili Union Version (SUV)

20. Amlaaniye babaye au mamaye,Taa yake itazimika katika giza kuu.

21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.

22. Usiseme, Mimi nitalipa mabaya;Mngojee BWANA, naye atakuokoa.

23. Vipimo mbalimbali ni chukizo kwa BWANA;Tena mizani ya hila si njema.

24. Mwenendo wa mtu watoka kwa BWANA;Basi, awezaje mtu kuelewa na njia yake?

25. Ni mtego, mtu aseme kwa haraka, Kitu hiki ni wakfu;Na baada ya kuweka nadhiri kuuliza-uliza habari.

26. Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki;Naye hulipitisha gurudumo la kupuria juu yao.

27. Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA;Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.

Mit. 20