14. Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi;Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.
15. Dhahabu iko, na marijani tele;Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani.
16. Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoze rehani aliye mdhamini wa wageni.
17. Chakula cha uongo ni kitamu kwa mtu;Lakini halafu kinywa chake kitajaa changarawe.
18. Kila kusudi huthibitika kwa kushauriana;Na kwa shauri la akili fanya vita.
19. Mwenye kitango akisingizia hufunua siri;Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.
20. Amlaaniye babaye au mamaye,Taa yake itazimika katika giza kuu.
21. Urithi uliopatikana mwanzo kwa haraka,Mwisho wake, lakini, hautabarikiwa.