Mit. 2:9-15 Swahili Union Version (SUV)

9. Ndipo utakapofahamu haki na hukumu,Na adili, na kila njia njema.

10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;

11. Busara itakulinda;Ufahamu utakuhifadhi.

12. Ili kukuokoa na njia ya uovu,Na watu wanenao yaliyopotoka;

13. Watu waziachao njia za unyofu,Ili kuziendea njia za giza;

14. Wafurahio kutenda mabaya;Wapendezwao na upotoe wa waovu;

15. Waliopotoka katika njia zao;Walio wakaidi katika mapito yao.

Mit. 2