10. Maana hekima itaingia moyoni mwako,Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;
11. Busara itakulinda;Ufahamu utakuhifadhi.
12. Ili kukuokoa na njia ya uovu,Na watu wanenao yaliyopotoka;
13. Watu waziachao njia za unyofu,Ili kuziendea njia za giza;
14. Wafurahio kutenda mabaya;Wapendezwao na upotoe wa waovu;
15. Waliopotoka katika njia zao;Walio wakaidi katika mapito yao.
16. Ili kuokoka na malaya,Naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake;
17. Amwachaye rafiki wa ujana wake,Na kulisahau agano la Mungu wake.