Mit. 2:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu,Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2. Hata ukatega sikio lako kusikia hekima,Ukauelekeza moyo wako upate kufahamu;

3. Naam, ukiita busara,Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4. Ukiutafuta kama fedha,Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5. Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA,Na kupata kumjua Mungu.

6. Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima;Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;

Mit. 2