Mit. 19:12-19 Swahili Union Version (SUV)

12. Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;Bali hisani yake kama umande juu ya majani.

13. Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye;Na ugomvi wa mke kama kutona-tona daima.

14. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye;Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na BWANA.

15. Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito;Na nafsi yake mvivu itaona njaa.

16. Yeye aihifadhiye amri huihifadhi nafsi yake;Bali yeye asiyeziangalia njia zake atakufa.

17. Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA;Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

18. Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini;Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.

19. Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake,Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.

Mit. 19