Mit. 19:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.

2. Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa;Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.

3. Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake;Na moyo wake hununa juu ya BWANA.

4. Utajiri huongeza rafiki wengi;Bali maskini hutengwa na rafiki yake.

5. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Wala asemaye uongo hataokoka.

Mit. 19