1. Afadhali maskini aendaye katika unyofu wake,Kuliko mpotofu wa midomo aliye mpumbavu.
2. Tena si vizuri nafsi ya mtu ikose maarifa;Naye afanyaye haraka kwa miguu hutenda dhambi.
3. Upumbavu wa mtu hupotosha njia yake;Na moyo wake hununa juu ya BWANA.
4. Utajiri huongeza rafiki wengi;Bali maskini hutengwa na rafiki yake.
5. Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa;Wala asemaye uongo hataokoka.