9. Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,Ni ndugu yake aliye mharabu.
10. Jina la BWANA ni ngome imara;Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
11. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
12. Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
13. Yeye ajibuye kabla hajasikia,Ni upumbavu na aibu kwake.