1. Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe;Hushindana na kila shauri jema.
2. Mpumbavu hapendezwi na ufahamu;Ila moyo wake udhihirike tu.
3. Ajapo asiye haki, huja dharau pia;Na pamoja na aibu huja lawama.
4. Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.