Mit. 18:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe;Hushindana na kila shauri jema.

2. Mpumbavu hapendezwi na ufahamu;Ila moyo wake udhihirike tu.

3. Ajapo asiye haki, huja dharau pia;Na pamoja na aibu huja lawama.

4. Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.

Mit. 18