Mit. 17:8-12 Swahili Union Version (SUV)

8. Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;Kila kigeukapo hufanikiwa.

9. Afunikaye kosa hutafuta kupendwa;Bali yeye akashifuye neno hutenga rafiki.

10. Lawama hupenya moyoni mwa mwenye ufahamu,Kuliko mapigo mia moyoni mwa mpumbavu.

11. Mtu mwovu hataki neno ila kuasi tu;Kwa hiyo mjumbe mkali atatumwa kwake.

12. Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake,Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake.

Mit. 17