1. Afadhali mego kavu pamoja na utulivu,Kuliko nyumba yenye karamu nyingi pamoja na magomvi.
2. Mtumwa atendaye kwa busara atamtawala mwana atendaye mambo ya aibu;Tena atapata sehemu ya urithi kati ya ndugu.
3. Kalibuni kwa fedha, na tanuru kwa dhahabu;Bali BWANA huijaribu mioyo.