Mit. 16:5-11 Swahili Union Version (SUV)

5. Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA;Hakika, hatakosa adhabu.

6. Kwa rehema na kweli uovu husafishwa;Kwa kumcha BWANA watu hujiepusha na maovu.

7. Njia za mtu zikimpendeza BWANA,Hata adui zake huwapatanisha naye.

8. Afadhali mali kidogo pamoja na haki,Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.

9. Moyo wa mtu huifikiri njia yake;Bali BWANA huziongoza hatua zake.

10. Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme;Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.

11. Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya BWANA;Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.

Mit. 16