17. Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu;Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.
18. Kiburi hutangulia uangamivu;Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.
19. Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini,Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.
20. Atakayelitafakari neno atapata mema;Na kila amwaminiye BWANA ana heri.