Mit. 16:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu;Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.

18. Kiburi hutangulia uangamivu;Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.

19. Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini,Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.

20. Atakayelitafakari neno atapata mema;Na kila amwaminiye BWANA ana heri.

Mit. 16