16. Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu?Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.
17. Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu;Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.
18. Kiburi hutangulia uangamivu;Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.